Quantcast
Channel: Afya – Fikra Pevu
Viewing all articles
Browse latest Browse all 296

Utafiti Mpya wabaini Ubora zaidi wa Maziwa kwa Afya ya Ubongo wa Binadamu

$
0
0

UTAFITI wa hivi karibuni uliofanywa na Taasisi ya Tiba ya Chuo Kikuu cha Kansas cha nchini Marekani, umebainisha kuwepo uwezezekano wa uhusiano wa karibu kati ya matumizi ya maziwa na afya ya ubongo.

Kwa mujibu wa utafiti huo mpya kabisa, matumizi ya maziwa mara kwa mara unaongeza kichocheo cha asili kinachopatikana kwenye ubongo wa mtu mzima mwenye afya njema, kichochea ambacho kitaalamu kinajulikana kama Glutathione.

Dk. In-Yung Choi ambaye ni Profesa Msaidizi wa Taasisi ya Tiba ya Chuo Kikuu hicho cha Kansas, ambaye pia hujishughulisha na mfumo wa fahamu, kwa ushirikiano na Dk Debra Sullivan, ambaye ni Profesa na Mwenyekiti wa Kitengo cha Lishe katika taasisi hiyo, ndio kwa pamoja wamebainisha hayo katika utafiti wao huo ambao FikraPevu imebahatika kuupata.

Matokeo ya utafiti wa madaktari wawili hao kuhusu maziwa, waliofanya kazi hiyo kwa kushirikiana, yamechapishwa na Jarida la The American Journal of Clinical Nutrition. Katika ushauri wao, wanasema kwamba unywaji wa maziwa, unaweza kuleta faida kwa mwili, hasa katika ubongo wa mwanadamu.

Kwa muda mrefu sasa imekuwa ikijulikana kwamba maziwa ni muhimu kwa ajili ya kuimarisha afya ya mifupa pamoja na nyama za miili ya binadamu.

Hata hivyo, Dk. Sullivan, katika matokeo ya utafiti wao huo ameandika: "Utafiti huu unaonyesha kwamba maziwa yanaweza kuwa muhimu kwa ubongo wako pia."

Katika utafiti wao huo, madaktari hao waliwauliza maswali washiriki 60, kwa kuhusisha ulaji wao pamoja na kupiga picha za ubongo wao, ambazo zilitumika kupima viwango vya Glutathione ambacho ndicho kichocheo chenye nguvu katika ubongo. Wengi wa washiriki hao, ambao walikuwa wamekunywa maziwa muda si mrefu kabla ya kufanyiwa utafiti huo, walionyesha kuwa na viwango vikubwa vya Glutathione kwenye ubongo wao. 

Kwa mujibu wa madaktari hao, kichocheo cha Glutathione kinaweza kusaidia kuondoa mkazo (Oxidative Stress), pamoja na kuondoa uharibifu unaoweza kusababishwa na utendaji wa kawaida wa ubongo.

Mara nyingi, mkazo huo huambatana na magonjwa tofauti na hali mbalimbali, kama vile magonjwa ya Alzheimer (ugonjwa wenye dalili za upungufu wa akili), Parkinson (ugonjwa wenye kuharibu mfumo wa fahamu pamoja na kuharibu ujongeaji/kutembea) na magonjwa mengine mengi yanayomkumba mwanadamu.

Ni maziwa yapi bora zaidi kati ya maziwa freshi na mtindi?

Maziwa yote, freshi na mtindi yana virutubishi muhimu, hasa vya protini, madini na vitamini. Kutokana na hali hiyo, mtu anaweza kutumia maziwa aina yoyote kati ya aina hizo mbili kutegemeana naa matumizi yake.

Hata hivyo, maziwa ya mtindi yanaelezwa kuyeyushwa zaidi kwa urahisi tumboni, na pia husaidia uyeyushwaji wa vyakula vingine pamoja na ufyonzwaji wa baadhi ya virutubishi vilivyomo ndani ya vyakula alavyo mwanadamu.

Kwa hiyo, maziwa ya mtindi yanapendekezwa zaidi na wataalam, hasa kwa wagonjwa kwa kuwa yanamsaidia mgonjwa kupata virutubishi vingi zaidi kwa haraka. Aidha, maziwa ya mtindi yana aina ya bakteria wazuri na salama ambao huweza kuzuia au kutibu fangasi katika mfumo wa chakula.

The post Utafiti Mpya wabaini Ubora zaidi wa Maziwa kwa Afya ya Ubongo wa Binadamu appeared first on Fikra Pevu.


Viewing all articles
Browse latest Browse all 296

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>