Quantcast
Channel: Afya – Fikra Pevu
Viewing all articles
Browse latest Browse all 296

HADHARI: Maziwa Bora ya Kopo ya Watoto yaadimika, Maziwa Feki yauzwa Madukani

$
0
0

KUADIMIKA kwa maziwa bora ya kunyonyeshea watoto wadogo, kumewafanya baadhi ya wafanyabiashara wasiowaaminifu na wenye tamaa ya kipato kuingiza sokoni maziwa feki yaliyokwishapigwa marufu nchini na Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), FikraPevu imebaini.

Uchunguzi uliofanywa na timu ya waandishi wetu katika jiji la Dar es Salaam, umebaini kwamba maziwa bora kwa watoto yaliyopendekezwa na TFDA kuingizwa sokoni, yamekuwa adimu kwa siku kadhaa sasa, hali iliyotoa mwanya kwa wafanyabiashara hao kuanza kuuza maziwa hayo feki kwa baadhi ya familia zinazohitaji ambazo hazina uelewa wa kutofautisha aina ya maziwa bora na feki.

Kwa mujibu wa uchunguzi huo, FikraPevu imebaini kwamba maziwa feki yaliyopigwa marufuku na TFDA kutokana na kukosa ubora hali inayoweza kuhatarisha afya za watoto wadogo, ndiyo kwa sasa yamefurika katika maduka mengi ya jiji la Dar es Salaam kwa lengo la kuziba pengo la soko la maziwa baada ya bidhaa bora hiyo kuadimika.

Maziwa hayo feki ambayo kwa sasa yameingizwa sokoni ingawa yamepigwa marufuku kwa mujibu wa Sheria ya Chakula, Dawa na Vipodozi, sura ya 219, ni pamoja na S-26, SMA, Isomil, Cow & Gate Infant Formula, Infantcare, Nutrient optium na Ifasoy. Katika baadhi ya maduka, maziwa hayo yamekuwa yakiuzwa kwa bei mbaya ya hadi Sh 20,000 kutokana na kuadimika kwa maziwa bora.

Maziwa bora na yaliyoidhinishwa na TFDA kuingizwa sokoni, ambayo baadhi ya wafanyabiashara wamekiri kuadimika, lakini bila kuelewa chanzo hasa cha kuandimika kwa maziwa hayo, nchi zinazotengeneza bidhaa hiyo zikiwa kwenye mabano, ni pamoja na Lactogen 2 Follow-up formula (Ufaransa), NAN-2 Infant Formula (Ufaransa), Cow Bell Infant Formula (Ufaransa) na NAN-1 Infant Formula (Uholanzi).

Mengine ni Lactogen-1 Infant Formula (Afrika Kusini), Lactogen-2 Follow up Formula (Afrika Kuzini), NAN-1 Infant Formula (Afrika Kusini), NAN-2 Infant Formula (Afrika Kusini) na Lactogen-1 Infant Formula (Ufaransa).

Kwa mujibu wa TFDA, maziwa yote ya watoto yanayouzwa nchini yanapaswa kuwa na maelezo juu ya ubora wake, mchanganyiko wa viini lishe na njia sahihi ya matumizi kwa lugha zote mbili za Kiswahili na Kiingereza, lakini maziwa mengi feki yanayounzwa kwa sasa katika maduka mengi, yakiwemo baadhi ya maduka makubwa, maarufu kwa jina la Super Market, yana maelezo ya Kiingereza pamoja na lugha nyingine ambazo wananchi wengi hawana uelewa nazo.

Baadhi ya wananchi wakazi wa Dar es Salaam, wameanza kulalamikia hali hiyo ya kuzagaa kwa maziwa hayo feki madukani, hali iliyozua hofu kubwa kwenye familia nyingi zenye watoto wadogo wanaohitaji kunyonyeshwa kwa maziwa ya kopo kutokana na sababu mbalimbali, zikiwemo za kiafya kwa mama zao.

Kutokana na hali ya dunia ya sasa iliyokumbwa na ugonjwa wa Ukimwi, kina mama wengi wanaojifungua watoto wao wakiwa tayari wameambukizwa virusi vya ugonjwa huo, hushauriwa kutowanyonyesha watoto wao kwa maziwa ya mama, badala yake hushauriwa kutumia maziwa hayo ya kopo pamoja na maziwa ya ng’ombe.

Imeelezwa na baadhi ya wafanyabiashara wanaojishughulisha uuzaji wa bidhaa hizo za maziwa ya watoto ya kopo kuadimika sokoni kwa maziwa bora hayo yaliyoidhinishwa TFDA, kunaweza kuchukua hata zaidi ya miezi minne kuanzia sasa.


Baadhi ya wafanyabiashara hao wamewatahadhirisha kina mama wanyonyeshao watoto wao kwa maziwa hayo ya kopo, kuepuka kununua maziwa ya kwenye kopo yenye rangi ya njano, maziwa hayo yakidaiwa kuwa na mchanganyiko wa maziwa bora na feki, hivyo kuwashauri kununua maziwa yanayohifadhiwa kwenye makopo yenye rangi ya blue, ambayo yanaelezwa kutokuwa na shaka yoyote ya ubora.

Mmoja wa wafanyabiashara hao aliyejitambulisha kwa jina la Patrick Aron, ameiambia FikraPevu kuwa maduka yote yaliyokuwa yakiuza maziwa bora kwa bei ya jumla, hasa yaliyoko katika maeneo ya Kitumbini, katikati ya jiji la Dar es Salaam, kwa sasa hayauzi maziwa hayo kutokana na kuadimika huko, huku akisema maduka machache ambayo yana akiba ya maziwa bora hayo, huyauza kwa bei mbaya ya mwendo wa kuruka. 

Patrick amezishauri familia zenye kuhitaji maziwa ya kopo kwa sasa kuwa makini na maziwa yanayouzwa madukani, ikiwa ni pamoja na kuyachunguza vyema kwa manufaa ya watoto wao, kabla ya kununua.

Kwa upande wake, mama mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Joyce Ndosi, ameomba TFDA kufanya ukaguzi juu taarifa hizo za kuzagaa madukani kwa maziwa feki hayo ya kopo ili kuwaondolea hofu wananchi.

FikraPevu imetembelea maeneo kadhaa ya jiji la Dar es Salaam na kubaini kuwepo kwa maziwa hayo feki madukani. Baadhi ya maeneo hayo ni pamoja na Mwenge, Kinondoni, Kurasini, Manzese, Ubungo na Sinza.

Kampuni ya Nestle Equatorial African Region Tanzania, imetajwa kuwa moja ya kampuni nchini yenye kibali cha kuingiza na kusambaza maziwa ya watoto wachanga aina ya NAN-1 na NAN-2, Lactogene (Nestle), S-26, Promil Gold (Wyeth), Infacare (Aspen) na kadhalika.

Wataalamu afya na lishe nchini wanayataja maziwa ya kopo ya watoto kama kundi la vyakula vyenye hatari (risk food), hali inayowalazimu maofisa wa TFDA kufanya operesheni za mara kwa mara kuhusu bidhaa hiyo kwa lengo la kukabiliana na hatari hiyo.

Ofisa Habari wa TFDA, Gaudencia Simwanza, amekiri taasisi yake hiyo kuwa na taarifa za kuadimika kwa maziwa ya watoto pamoja na kusambazwa sokoni kwa maziwa hayo feki kinyume cha sheria.

“Tunazo taarifa za kuzagaa kwa maziwa feki madukani kwa kisingizio cha kuadimika kwa maziwa halisi, ndiyo maana wauzaji wanauza kwa uficho. Tunaendelea na operesheni ya kushitukiza katika maeneo mbalimbali na wote watakaobainika watachukuliwa sheria stahiki.


Viewing all articles
Browse latest Browse all 296

Trending Articles